5 Juni 2025 - 16:34
“Nunua Pepo kwa Matendo Haya Machache” – Kwa Mujibu wa Qur’an na Hadithi

Qur’an (Al-Israa: 23): “Na watendee wema wazazi wawili.” Hili ni agizo la moja kwa moja kutoka kwa Allah - ni njia ya hakika ya kuelekea Peponi.

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA- Katika Uislamu, kuna matendo ambayo yameelezwa wazi kuwa ni njia za uhakika za kuingia peponi. Haya hapa ni baadhi ya matendo hayo muhimu:

1. Kuswali kwa Unyenyekevu

Mtume Muhammad (s.a.w) amesema:
"Amali ya kwanza kuhesabiwa Siku ya Kiyama ni swala. Ikiwa ni sahihi, amali nyingine pia zitakubaliwa."

2. Kuwatendea Wema Wazazi

Qur’an (Al-Israa: 23):
“Na watendee wema wazazi wawili.”
Hili ni agizo la moja kwa moja kutoka kwa Allah – ni njia ya hakika ya kuelekea Peponi.

3. Kumlisha Mhitaji

Imam Ja’far as-Sadiq (a.s) amesema:
"Atakaye mlisha Muumini, Allah atamlisha matunda ya Peponi."

4. Kusamehe na Kuachilia

Qur’an (Aali Imran: 134):
“Na wasamehevyo watu, na Allah huwapenda wafanyao wema.”
Wenye kusamehe ni wapenzi wa Allah na ni wakaaji wa Pepo.

5. Kusoma Qur’an

Mtume (s.a.w):
"Qur’an ni mwenye kushuhudia kwa anayesoma, na shuhuda yake itakubaliwa."
Kuwa na uhusiano wa karibu na Qur’an ni njia ya nuru kuelekea Peponi.

6. Kulinda Ulimi

Imam Ali (a.s) amesema:
"Ulimi ni ufunguo wa kheri na shari. Heri kwa anayelinda ulimi wake."

7. Kumkumbuka Allah Mara kwa Mara

Qur’an (Al-Ahzaab: 35):
“Wanaomkumbuka Allah kwa wingi – wanaume na wanawake – Allah amewaandalia msamaha na ujira mkubwa.”
Dhikri (kumuadhukuru Allah) ni njia ya uhakika ya kuelekea rehma na Pepo.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha